Kisanduku Cha Maulizo
◼ Je, Tunaweza Kusali Tunapoongoza Funzo la Biblia Tukiwa Wenye Kusimama Kwenye Mulango?
Kuna faida nyingi za kusali na mwanafunzi wa Biblia mbele ya kujifunza na tunapomaliza funzo. Tunaposali, tunamwomba Yehova roho yake ili itusaidie tunapojifunza. (Luka 11:13) Sala inamusaidia pia mwanafunzi wetu achukue funzo kwa uzito na anapotusikia tukisali yeye pia anajifunza jinsi ya kusali. (Luka 6:40) Kwa hiyo, tunapoanza kujifunza na mutu fulani ni vizuri tuanze kusali pamoja naye bila kukawia. Hata hivyo, kwa kuwa hali za watu zinaachana, mwenye kuongoza funzo anahitaji kutumia utambuzi ili kuamua ikiwa atasali ao hapana, anapoongoza funzo la Biblia wakiwa wenye kusimama kwenye mulango.
Jambo la maana ambalo tunapaswa kufikiria ni mahali ambapo funzo litafanyiwa. Ikiwa funzo linaongozwa mahali fulani panapowafanya muwe peke yenu ao mahali watu hawapitepite, sala fupi inaweza kutolewa ili kuanza na kumaliza funzo linaloongozwa kwa ukawaida hata tukiwa wenye kusimama kwenye mulango. Lakini jambo hilo linapaswa kufanywa bila kuvutia uangalifu wa watu. Na ikiwa kusali kutavutia uangalifu wa watazamaji ao kutamufanya mwanafunzi asijisikie vizuri, itakuwa vizuri kungoja mupaka funzo linapoanza kufanywa katika hali ao mahali panapofaa. Iwe tunajifunzia mahali gani, tunapaswa kutumia utambuzi ili kuamua ni wakati gani tutaanza kusali pamoja na mwanafunzi.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 3, 2005, ukurasa wa 6.