Zaburi
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
83 Ee Mungu, usinyamaze;+
Usikae kimya wala kutulia, Ee Mungu.
3 Kwa hila wanapanga njama kwa siri dhidi ya watu wako;
Wanapanga njama dhidi ya watu wako unaowathamini.*
4 Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+
Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”
5 Kwa umoja wanatunga mbinu;*
6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,
9 Watendee kama ulivyoitendea Midiani,+
Kama ulivyomtendea Sisera na Yabini kwenye kijito cha* Kishoni.+
10 Waliangamizwa kule En-dori;+
Wakawa mbolea juu ya ardhi.
11 Wafanye viongozi wao wawe kama Orebu na Zeebu+
Na wakuu* wao kama Zeba na Zalmuna,+
12 Kwa maana walisema: “Na tuimiliki nchi ambamo Mungu anakaa.”
13 Ee Mungu wangu, wafanye wawe kama mchongoma unaopeperushwa,*+
Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo.
14 Kama moto unaoteketeza kabisa msitu,
Kama mwali wa moto unaounguza milima,+
15 Wafuatie vivyo hivyo kwa tufani yako+
Na kuwaogopesha kwa dhoruba yako ya upepo.+
16 Funika nyuso zao kwa aibu,*
Ili walitafute jina lako, Ee Yehova.