-
Mambo ya Walawi 18:24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 “‘Msijichafue kwa kufanya jambo lolote kati ya mambo hayo, kwa maana mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejichafua kwa mambo hayo yote.+
-
-
Hesabu 35:33, 34Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
33 “‘Msiichafue nchi mnayoishi ndani yake, kwa sababu damu inachafua nchi,+ na hakuna msamaha kwa ajili ya damu iliyomwagwa nchini isipokuwa kwa kumwaga damu ya yule aliyeimwaga.+ 34 Msiitie unajisi nchi mnayoishi ndani yake, ambamo ninakaa; kwa maana mimi, Yehova, ninakaa miongoni mwa Waisraeli.’”+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 33:9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Manase aliendelea kuwapotosha watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, akasababisha watende mambo maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya Waisraeli.+
-