Zaburi
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Kikumbusho. Muziki wa Asafu.+
80 Ee Mchungaji wa Israeli, sikiliza,
Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi la kondoo.+
4 Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mpaka lini kuwa na hasira kali kuelekea* sala ya watu wako?+
5 Unawalisha machozi kama mkate,
Nawe unawanywesha machozi kupita kiasi.
6 Unawaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;
Maadui wetu wanaendelea kutudhihaki wapendavyo.+
7 Ee Mungu wa majeshi, turudishe;
Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+
8 Uliufanya mzabibu+ uondoke Misri.
Uliyafukuza mataifa na kuupanda.+
9 Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,
Nao ukatia mizizi na kujaa nchini.+
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 Matawi yake yalienea mpaka baharini,
Na machipukizi yake mpaka kwenye Mto Efrati.+
12 Kwa nini umebomoa kuta za mawe za shamba la mzabibu huo,+
Hivi kwamba wote wanaopita karibu nao wanachuma matunda yake?+
13 Nguruwe wa mwituni wanauharibu,
Na wanyama wa porini wanaula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, rudi tafadhali.
Tazama chini kutoka mbinguni uone!
Utunze mzabibu huu,+
15 Shina* ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+
Na umtazame mwana ambaye umemtia nguvu* kwa ajili yako mwenyewe.+
16 Umechomwa moto,+ umekatwa.
Wanaangamia kwa kemeo lako.*
17 Mkono wako na umtegemeze mwanamume aliye kwenye mkono wako wa kuume,
Mwana wa binadamu uliyemtia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Kisha hatutageuka kutoka kwako.
Tuhifadhi hai, ili tuliitie jina lako.
19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, turudishe;
Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+