Ayubu
8 Naye Bildadi Mshua+ akajibu, akasema:
2 “Utaendelea kusema mambo haya mpaka wakati gani,+
Wakati maneno ya kinywa chako ni upepo mtupu wenye nguvu?+
4 Ikiwa wana wako mwenyewe wamemtendea dhambi,
Hivi kwamba anawaacha waingie mkononi mwa maasi yao,
5 Ikiwa wewe mwenyewe utamtafuta Mungu,+
Na ikiwa utamwomba kwa bidii kibali Mweza-Yote,
6 Ikiwa wewe ni safi na mnyoofu,+
Kufikia sasa angeamka kwa ajili yako
Naye hakika angerudisha makao yako ya uadilifu.
7 Pia, huenda ikawa mwanzo wako ulikuwa jambo dogo,
Lakini mwisho wako baadaye ungekuwa mkubwa sana.+
8 Kwa kweli, tafadhali uliza wale wa kizazi cha zamani,+
Nawe uelekeze fikira zako kwenye mambo ambayo baba zao waliyachunguza.+
10 Je, wao wenyewe hawatakufundisha, wakuambie,
Na je, hawatatoa maneno kutoka moyoni mwao?
11 Je, mmea wa mafunjo+ utakua uwe mrefu mahali pasipo na majimaji?
Je, tete litakua liwe kubwa bila maji?
15 Ataegemea juu ya nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;
Ataishika, lakini haitadumu.
17 Mizizi yake husokotana ndani ya rundo la mawe,
Anatazama nyumba ya mawe.