Ayubu
7 “Je, duniani hakuna kazi ya lazima+ kwa mwanadamu anayeweza kufa,
Na je, siku zake si kama siku za mfanyakazi wa kukodiwa?+
2 Kama mtumwa, yeye hupumua kwa kutamani kivuli,+
Naye hungojea mshahara wake kama mfanyakazi wa kukodiwa.+
4 Wakati ninapolala chini nimesema, ‘Nitaamka wakati gani?’+
Na jioni inapoisha, pia nimejawa na ukosefu wa utulivu mpaka mapambazuko ya asubuhi.
5 Nyama yangu imefunikwa na funza+ na madonge ya mavumbi;+
Ngozi yangu imefanyiza vikoko na kuyeyuka.+
6 Siku zangu zimepita upesi+ kuliko chombo cha mfumaji,
Nazo hufikia mwisho katika hali ya ukosefu wa tumaini.+
9 Wingu kwa hakika hufikia mwisho wake na kwenda zake;
Ndivyo ambavyo yeye anayeshuka katika Kaburi* hatapanda juu.+
11 Mimi pia sitazuia kinywa changu.
Nitasema katika taabu ya roho yangu;
Nitahangaikia uchungu wa nafsi yangu!+
13 Niliposema, ‘Kitanda changu kitanifariji,
Kitanda changu kitanisaidia kuchukua hangaiko langu,’
14 Hata hivyo umeniogopesha kwa ndoto,
Nawe kupitia maono hunifanya nishtuke kwa woga,
15 Hivi kwamba nafsi yangu inachagua kusongwa pumzi,
Kifo+ badala ya mifupa yangu.
16 Nimekataa huo;+ sitaishi mpaka wakati usio na kipimo.
Niache mimi, kwa sababu siku zangu ni upepo wa pumzi.+
17 Mwanadamu anayeweza kufa+ ni kitu gani ili kwamba umlee,
Na ndipo uuweke moyo wako juu yake,
18 Na ndipo umkazie uangalifu kila asubuhi,
Ndipo umjaribu kila dakika?+