Waebrania
8 Sasa kuhusu mambo yanayozungumzwa jambo kuu ni hili: Sisi tuna kuhani wa cheo cha juu wa namna hii, naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukuu katika mbingu, 2 mtumishi wa watu wote wa mahali patakatifu na wa hema la kweli, ambalo Yehova alisimamisha, wala si mwanadamu. 3 Kwa maana kila kuhani wa cheo cha juu huwekwa rasmi ili kuzitoa zawadi na dhabihu pia; kwa sababu hiyo ilikuwa lazima kwa huyu pia kuwa na kitu fulani cha kutoa. 4 Sasa, kama angekuwa juu ya dunia, hangekuwa kuhani, kukiwa na watu ambao huzitoa zawadi kulingana na Sheria, 5 lakini watu wanaotoa utumishi mtakatifu katika kiwakilishi cha mfano wa uhalisi na kivuli cha vitu vya kimbingu; kama vile Musa, alipokuwa karibu kufanya hema kwa ukamili, alivyopewa amri ya kimungu: Kwa maana yeye asema: “Angalia uvifanye vitu vyote kwa kufuatisha kiolezo chavyo ulichoonyeshwa katika mlima.” 6 Lakini sasa Yesu amepata utumishi wa watu wote ulio bora kabisa zaidi, hivi kwamba kwa kulingana yeye ni mpatanishi pia wa agano lililo bora, ambalo limethibitishwa kisheria juu ya ahadi zilizo bora.
7 Kwa maana ikiwa agano hilo la kwanza lingalikuwa bila hitilafu, hakuna mahali ambapo pangalitafutwa kwa la pili; 8 kwa maana yeye atafuta kosa katika hao watu asemapo: “‘Tazama! Kuna siku zinazokuja,’ asema Yehova, ‘nami hakika nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na pamoja na nyumba ya Yuda; 9 si kulingana na agano nililofanya pamoja na baba zao wa zamani katika siku ambayo nilishika mkono wao ili kuwaleta kutoka nchi ya Misri, kwa sababu hawakuendelea katika agano langu, hivi kwamba nikakoma kuwajali,’ asema Yehova.”
10 “‘Kwa maana hili ndilo agano nitakaloagana pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova. ‘Hakika mimi nitatia sheria zangu katika akili yao, na katika mioyo yao nitaziandika. Nami hakika nitakuwa Mungu wao, nao wenyewe watakuwa watu wangu.
11 “‘Nao hawatafundisha kwa vyovyote kila mmoja raia mwenzake na kila mmoja ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!” Kwa maana wote watanijua, tangu mdogo zaidi sana mpaka mkubwa zaidi sana kati yao. 12 Kwa maana nitakuwa mwenye rehema kwa vitendo vyao visivyo vya uadilifu, nami kwa vyovyote sitakumbuka tena dhambi zao.’”
13 Kwa kusema kwake “agano jipya” amefanya la hapo zamani kuwa kuukuu. Sasa lile lifanywalo kuwa kuukuu na linalozeeka liko karibu kutoweka.