28 Wanaume, wanabiashara Wamidiani,+ wakapitia hapo. Basi wakamvuta na kumpandisha Yosefu kutoka katika lile shimo la maji+ kisha wakamuuza kwa wale Waishmaeli kwa vipande 20 vya fedha.+ Mwishowe wanabiashara hao wakampeleka Yosefu Misri.
21 Nao wakaanza kusemezana: “Bila shaka tuna hatia kuhusiana na ndugu yetu,+ kwa sababu tuliona nafsi yake ikitaabika alipotuomba kwa bidii tumwonee huruma, lakini sisi hatukusikiliza. Ndiyo sababu taabu hii imetupata.”+