35 Naye akafanya pazia+ la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa. Akalitia makerubi kwa kazi ya mtarizi.+
21 Halafu akaleta lile Sanduku ndani ya maskani na kuweka lile pazia+ la kusitiri mahali pake na kufunga njia ya kuingia penye sanduku la ushuhuda,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
2 Na Yehova akamwambia Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, asiwe akija nyakati zote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya Sanduku, asije akafa;+ kwa sababu nitaonekana katika wingu+ juu ya kifuniko+ hicho.