19 Na yule mtu aliye safi atayatapanya juu ya yule asiye safi siku ya tatu na siku ya saba na kumtakasa kutokana na dhambi yake siku ya saba;+ naye atayafua mavazi yake na kuoga katika maji, naye atakuwa safi jioni.
20 “‘Lakini mtu asiye safi na ambaye hatajitakasa, basi, nafsi hiyo lazima ikatiliwe mbali+ kutoka katikati ya kutaniko, kwa sababu amepatia unajisi patakatifu pa Yehova. Maji ya kutakasa hayakunyunyizwa juu yake. Yeye si safi.