Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Sitawafukuza kutoka mbele yako kwa mwaka mmoja, ili nchi isiwe mahame yenye ukiwa nao wanyama wa mwituni waongezeke kwelikweli juu yako.+

  • Hesabu 33:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 “‘Hata hivyo, ikiwa hamtawafukuzia mbali wakaaji wa nchi hiyo kutoka mbele yenu,+ basi wale mtakaoacha watakuwa kama michomo katika macho yenu na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika nchi ambamo mtakuwa mkikaa.+

  • Waamuzi 1:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu;+ bali Wayebusi wanaendelea kukaa pamoja na wana wa Benyamini katika Yerusalemu mpaka leo.+

  • Waamuzi 2:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kwa hiyo Yehova akayaacha mataifa hayo yabaki kwa kutoyafukuza upesi,+ wala hakuyatia mkononi mwa Yoshua.

  • Waamuzi 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Nao wakaendelea kutumika kama vyombo vya kujaribu+ Israeli ili kujua kama wangetii amri za Yehova ambazo alikuwa ameamuru baba zao kupitia Musa.+

  • Waamuzi 19:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Walipokuwa karibu na Yebusi, kwa kuwa mchana ulikuwa umeendelea sana,+ yule mtumishi akamwambia bwana wake: “Haya, tafadhali, na tugeuke kando tuingie katika jiji hili la Wayebusi,+ tulale humo usiku kucha.”

  • 2 Samweli 5:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Basi mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kupigana na Wayebusi+ wanaokaa katika nchi, nao wakaanza kumwambia Daudi: “Wewe hutaingia humu, lakini bila shaka vipofu na vilema watakufukuza,”+ wao walikuwa wakifikiri: “Daudi hataingia humu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki