Kutoka
23 “Usieneze habari isiyo ya kweli.+ Usishirikiane na mtu mwovu kwa kuwa shahidi anayepanga jeuri.+ 2 Usiufuate umati kwa ajili ya makusudio maovu;+ wala usishuhudie juu ya ubishi ili kugeuka kando pamoja na umati kwa kusudi la kupotosha haki.+ 3 Na kwa ajili ya mtu wa hali ya chini, usionyeshe upendeleo katika ubishi wake.+
4 “Ukikutana na ng’ombe-dume au punda wa adui yako akipotea, lazima umrudishe kwake.+ 5 Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia akiwa amelala chini ya mzigo wake, basi lazima ujizuie usimwache. Lazima utamfungua pamoja naye.+
6 “Usipotoshe uamuzi wa hukumu wa mtu wako aliye maskini katika ubishi wake.+
7 “Utakaa mbali na neno la uwongo.+ Nawe usimuue mtu asiye na hatia na yule aliye mwadilifu, kwa maana sitamtangaza mwovu kuwa mwadilifu.+
8 “Usikubali rushwa, kwa maana rushwa hupofusha watu wanaoona vizuri na inaweza kupotosha maneno ya watu waadilifu.+
9 “Nawe usimkandamize mkaaji mgeni,+ kwa maana ninyi wenyewe mmeijua nafsi ya mkaaji mgeni, kwa sababu mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+
10 “Na kwa miaka sita utapanda mbegu katika shamba lako nawe utakusanya mazao yake.+ 11 Lakini mwaka wa saba utaliacha bila kulimwa nawe utaliacha lipumzike,+ nao maskini wa watu wako watakula kutokana nalo; nacho kile ambacho wataacha kitaliwa na wanyama wa mwituni.+ Hivyo ndivyo utakavyofanya na shamba lako la mizabibu na shamba lako la mizeituni.
12 “Siku sita utafanya kazi yako;+ lakini siku ya saba utaacha, ili ng’ombe-dume wako na punda wako wapate kupumzika na mwana wa kijakazi wako na mkaaji mgeni wapate kujiburudisha.+
13 “Nanyi mtajilinda kuhusiana na yote hayo ambayo nimewaambia ninyi;+ nanyi msilitaje jina la miungu mingine. Lisisikiwe kinywani mwako.+
14 “Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sherehe.+ 15 Utaishika sherehe ya keki zisizo na chachu.+ Utakula keki zisizo na chachu+ siku saba, kama vile ambavyo nimekuamuru, wakati uliowekwa katika mwezi wa Abibu,+ kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. Nao wasionekane mbele zangu mikono mitupu.+ 16 Pia, sherehe ya mavuno ya matunda ya kwanza yaliyoiva+ ya kazi zenu, ya vitu mnavyopanda shambani;+ na sherehe ya kukusanya mwishoni mwa mwaka, wakati ambapo mnakusanya kazi zenu kutoka shambani.+ 17 Pindi tatu katika mwaka kila mwanamume wa kwako ataonekana mbele za uso wa Bwana wa kweli, Yehova.+
18 “Msitoe dhabihu damu ya dhabihu yangu pamoja na kitu kilicho na chachu. Nayo mafuta ya sherehe yangu yasikae usiku kucha mpaka asubuhi.+
19 “Yaliyo bora zaidi kati ya matunda ya kwanza yaliyoiva ya udongo wako utayaleta katika nyumba ya Yehova Mungu wako.+
“Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+
20 “Tazama, ninamtuma malaika+ mbele yako ili akuongoze barabarani na kukuingiza mahali ambapo nimetayarisha.+ 21 Jiangalie kwa sababu yake na kuitii sauti yake. Usijiendeshe kwa kumwasi yeye, kwa maana hatawasamehe kosa lenu;+ kwa sababu jina langu limo ndani yake. 22 Hata hivyo, ukiitii sauti yake kabisa na kwa kweli ufanye yote nitakayosema,+ basi hakika nitawaonyesha adui zako uadui na kuwasumbua wale wanaokusumbua.+ 23 Kwa maana malaika wangu ataenda mbele yako naye kwa kweli atakuongoza kwa Waamori na Wahiti na Waperizi na Wakanaani, na Wahivi na Wayebusi, nami hakika nitawafutilia hao mbali.+ 24 Usiinamie miungu yao wala kuchochewa kuitumikia, wala usifanyize chochote kilicho kama kazi zao,+ bali lazima utawaangusha nawe lazima uzivunje nguzo zao takatifu.+ 25 Nanyi mtamtumikia Yehova Mungu wenu,+ naye hakika ataubariki mkate wako na maji yako;+ nami kwa kweli nitageuzia mbali ugonjwa kutoka katikati yako.+ 26 Wala hakutakuwa na mwanamke ambaye mimba yake itatoka wala mwanamke tasa katika nchi yako.+ Nitafanya hesabu ya siku zako itimie.+
27 “Na nitatuma mbele yako hali ya kuniogopa,+ nami hakika nitawavuruga watu wote utakaoingia katikati yao, nami kwa kweli nitakupa shingo za adui zako wote.+ 28 Nami nitaituma mbele yako hisia ya kuvunjika moyo,+ nayo itawafukuzia mbali Wahivi, Wakanaani na Wahiti kutoka mbele yako.+ 29 Sitawafukuza kutoka mbele yako kwa mwaka mmoja, ili nchi isiwe mahame yenye ukiwa nao wanyama wa mwituni waongezeke kwelikweli juu yako.+ 30 Nitawafukuza kutoka mbele yako hatua kwa hatua, mpaka uongezeke na kuimiliki nchi hiyo kabisa.+
31 “Nami nitauweka mpaka wako kutoka Bahari Nyekundu hadi bahari ya Wafilisti na kutoka nyikani hadi kwenye Mto;+ kwa sababu nitawaweka wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, na hakika wewe utawafukuzia mbali kutoka mbele yako.+ 32 Hutafanya agano pamoja nao au miungu yao.+ 33 Wasikae katika nchi yako, wasije wakakufanya unitendee dhambi. Ikiwa utaitumikia miungu yao, itakuwa mtego kwako.”+