5 Usiviinamie wala kushawishiwa kuvitumikia,+ kwa sababu mimi Yehova Mungu wako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili,+ na ambaye huleta adhabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la akina baba, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne, kwa wale wanaonichukia;+
3 Jinsi inavyofanya nchi ya Misri ambamo mlikaa, msifanye;+ na jinsi inavyofanya nchi ya Kanaani, ambamo nitawaleta, msifanye;+ na katika sheria zao msitembee.
30 Jiangalie usije ukanaswa na kuwafuata,+ baada ya wao kuangamizwa kutoka mbele yako, nawe usije ukauliza kuhusu miungu yao, na kusema, ‘Mataifa haya yalikuwa yakiitumikiaje miungu yao? Nami, naam, mimi nitafanya vivyo hivyo.’
2 Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na machukizo+ ya mataifa ambayo Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+