24 Usiinamie miungu yao wala kuchochewa kuitumikia, wala usifanyize chochote kilicho kama kazi zao,+ bali lazima utawaangusha nawe lazima uzivunje nguzo zao takatifu.+
30 Jiangalie usije ukanaswa na kuwafuata,+ baada ya wao kuangamizwa kutoka mbele yako, nawe usije ukauliza kuhusu miungu yao, na kusema, ‘Mataifa haya yalikuwa yakiitumikiaje miungu yao? Nami, naam, mimi nitafanya vivyo hivyo.’
2 Yehova amesema hivi: “Msijifunze njia ya mataifa hata kidogo,+ wala msiingiwe na hofu kutokana na ishara za mbinguni, kwa sababu mataifa yanaingiwa na hofu kutokana nazo.+