23 Kwa maana malaika wangu ataenda mbele yako naye kwa kweli atakuongoza kwa Waamori na Wahiti na Waperizi na Wakanaani, na Wahivi na Wayebusi, nami hakika nitawafutilia hao mbali.+
63 Lakini wale Wayebusi+ waliokuwa wakikaa katika Yerusalemu,+ wana wa Yuda hawakuweza kuwafukuza;+ basi hao Wayebusi wanaendelea kukaa pamoja na wana wa Yuda katika Yerusalemu mpaka leo hii.
8 Zaidi ya hayo, wana wa Yuda wakaendelea kupigana vita na jiji la Yerusalemu+ nao wakaliteka, wakalipiga kwa makali ya upanga, kisha wakateketeza jiji hilo kwa moto.
21 Na wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu;+ bali Wayebusi wanaendelea kukaa pamoja na wana wa Benyamini katika Yerusalemu mpaka leo.+