22 Lakini Hana hakupanda,+ kwa maana alikuwa amemwambia mume wake: “Mara mvulana huyu atakapoachishwa kunyonya,+ nitampeleka, naye ataonekana mbele za Yehova na kukaa huko mpaka wakati usio na kipimo.”+
24 Kwa hiyo mara tu alipomwachisha kunyonya, akapanda pamoja naye, pamoja na ng’ombe-dume wa miaka mitatu na efa moja ya unga na mtungi mkubwa wa divai,+ naye akaingia ndani ya nyumba ya Yehova katika Shilo.+ Na huyo mvulana alikuwa pamoja naye.