10 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Hakika mimi nitarudi kwako mwaka ujao wakati huu, na, tazama! Sara mke wako atapata mwana.”+ Basi Sara alikuwa akisikiliza kwenye mwingilio wa hema, nao ulikuwa nyuma ya mwanamume huyo.
20 Kwa hiyo ikawa mwishoni mwa mwaka kwamba Hana akachukua mimba, akamzaa mwana, akamwita jina+ lake Samweli, kwa maana alisema, “Nimemwomba kutoka kwa Yehova.”+
16 Kisha akasema: “Mwaka ujao wakati huu uliowekwa utakuwa unamkumbatia mwana.”+ Lakini mwanamke huyo akasema: “Hapana, bwana wangu, ewe mtu wa Mungu wa kweli! Usimwambie uwongo mjakazi wako.”
13 Hata hivyo, malaika akamwambia: “Usiogope, Zekaria, kwa sababu dua yako imekubaliwa,+ na mke wako Elisabeti atamzaa mwana wako, nawe utamwita jina lake Yohana.+