3 Na mfalme akaendelea kusema: “Je, hakuna kabisa mtu wa nyumba ya Sauli, ili nimwonyeshe fadhili zenye upendo za Mungu?”+ Hivyo Siba akamwambia mfalme: “Bado kuna mwana wa Yonathani, mwenye kulemaa miguu.”+
7 Na Daudi akaendelea kumwambia: “Usiogope, kwa maana hakika nitakuonyesha fadhili zenye upendo+ kwa ajili ya Yonathani baba yako;+ nami nitakurudishia mashamba+ yote ya Sauli babu yako, nawe utakula mkate mezani pangu sikuzote.”+