8 Nami ninashuka ili kuwakomboa kutoka katika mkono wa Wamisri+ na kuwatoa katika nchi hiyo mpaka kwenye nchi nzuri na kubwa, nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kwa Wakanaani na Wahiti na Waamori na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+
5 Na sasa ikiwa mtaitii+ sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano+ langu, ndipo hakika mtakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu,+ kwa sababu dunia nzima ni yangu.+
9 Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha.+ Na mjumbe wake binafsi akawaokoa.+ Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa,+ naye akawainua na kuwachukua siku zote za zamani za kale.+