15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amemwambia Tiro hivi, ‘Inapotokea sauti ya kuanguka kwako, wakati ambapo aliyetiwa majeraha ya kufisha atakapougua, wakati ambapo kutakuwapo mauaji yenye machinjo katikati yako, je, visiwa havitatikisika?+
“ ‘Wewe unayekaa katika malango ya bahari,+ mwanamke mfanya-biashara wa vikundi vya watu wa visiwa vingi,+ Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ee Tiro, wewe mwenyewe umesema, ‘Mimi ni mkamilifu wa uzuri.’+