10 Basi jueni kwamba hakuna neno lolote la Yehova litakaloanguka chini+ bila kutimizwa ambalo Yehova amesema juu ya nyumba ya Ahabu;+ na Yehova mwenyewe amefanya aliyoyasema kupitia Eliya mtumishi wake.”+
11 Tena Yehu akaendelea kuwapiga na kuwaua wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu katika Yezreeli na watu wake wote walio mashuhuri+ na rafiki zake na makuhani+ wake, mpaka alipokuwa amewaangamiza watu wake wote, bila kuacha mwokokaji yeyote abaki.+