2 Wafalme
10 Basi Ahabu alikuwa na wana 70+ katika Samaria.+ Kwa hiyo Yehu akaandika barua, akazituma Samaria kwa wakuu+ wa Yezreeli, wanaume wazee+ na watunzaji wa Ahabu, na kusema: 2 “Basi, sasa, wakati ule barua hii inapowafikia ninyi, mnao wana wa bwana wenu pamoja nanyi, na mnayo magari ya vita na farasi+ pamoja nanyi na jiji lenye ngome na silaha. 3 Nanyi mwone ni nani aliye bora zaidi na mnyoofu zaidi kati ya wana wa bwana wenu, mkamweke yeye juu ya kiti cha ufalme cha baba yake.+ Halafu mpiganie nyumba ya bwana wenu.”
4 Nao wakaogopa sana, wakaanza kusema: “Tazama! Wafalme wawili+ hawakusimama mbele yake, nasi tutasimamaje?”+ 5 Kwa hiyo yule aliyekuwa juu ya nyumba na yule aliyekuwa juu ya jiji na wanaume wazee na watunzaji+ wakatuma ujumbe kwa Yehu, wakisema: “Sisi ni watumishi wako, na kila jambo unalotuambia tutafanya. Hatutamfanya yeyote kuwa mfalme. Fanya yaliyo mema machoni pako.”
6 Ndipo akawaandikia barua ya pili, na kusema: “Ikiwa ninyi ni wangu,+ nanyi mnaitii sauti yangu, chukueni vichwa vya hao wana+ wa bwana wenu, mje kwangu kesho wakati kama huu katika Yezreeli.”+
Basi wana wa mfalme, watu 70, walikuwa na wanaume mashuhuri wa jiji waliokuwa wakiwalea. 7 Na ikawa kwamba mara tu barua ile ilipowafikia, wakawachukua wale wana wa mfalme na kuwachinja, watu 70,+ kisha wakaviweka vichwa vyao ndani ya vikapu, wakampelekea kule Yezreeli. 8 Kisha yule mjumbe+ akaingia na kumwambia: “Wamevileta vichwa+ vya wana wa mfalme.” Kwa hiyo akasema: “Viwekeni katika mafungu mawili kwenye mwingilio wa lango mpaka asubuhi.”+ 9 Na ikawa kwamba wakati wa asubuhi akaondoka. Kisha akasimama tuli na kuwaambia watu wote: “Ninyi ni waadilifu.+ Tazama, mimi mwenyewe nilipanga hila+ juu ya bwana wangu, nami nikamuua;+ lakini ni nani aliyewapiga na kuwaua hawa wote? 10 Basi jueni kwamba hakuna neno lolote la Yehova litakaloanguka chini+ bila kutimizwa ambalo Yehova amesema juu ya nyumba ya Ahabu;+ na Yehova mwenyewe amefanya aliyoyasema kupitia Eliya mtumishi wake.”+ 11 Tena Yehu akaendelea kuwapiga na kuwaua wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu katika Yezreeli na watu wake wote walio mashuhuri+ na rafiki zake na makuhani+ wake, mpaka alipokuwa amewaangamiza watu wake wote, bila kuacha mwokokaji yeyote abaki.+
12 Naye akasimama na kuingia, kisha akaenda zake Samaria. Nyumba ya kufungia ya wachungaji ilikuwa njiani. 13 Na Yehu akakutana na ndugu+ za Ahazia+ mfalme wa Yuda. Alipowaambia, “Ninyi ni nani?” ndipo wakasema: “Sisi ni ndugu za Ahazia, nasi tuko njiani kwenda kuuliza kama ni salama kwa wana wa mfalme na kwa wana wa malkia.” 14 Mara moja akasema: “Wakamateni wakiwa hai!”+ Kwa hiyo wakawakamata wakiwa hai, wakawachinja kando ya tangi la maji la ile nyumba ya kufungia, watu 42, naye hakumwacha hata mmoja wao abaki.+
15 Alipokuwa akienda kutoka hapo, akakutana na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu+ akija kumpokea. Alipombariki,+ akamwambia: “Je, moyo wako ni mnyoofu kunielekea mimi, kama vile moyo wangu ulivyo kuuelekea moyo wako?”+
Ndipo Yehonadabu akasema: “Ndiyo.”
“Ikiwa ndivyo, nipe mkono wako.”
Kwa hiyo akampa mkono wake. Basi akampandisha ndani ya gari pamoja naye.+ 16 Kisha akasema: “Enda pamoja nami, utazame jinsi ambavyo sivumilii ushindani+ wowote kumwelekea Yehova.” Nao wakaendelea kumwendesha pamoja naye katika gari lake la vita. 17 Mwishowe akafika Samaria. Sasa akaanza kuwapiga na kuwaua wote waliobaki wa Ahabu katika Samaria, mpaka akawaangamiza,+ kulingana na neno la Yehova alilomwambia Eliya.+
18 Tena Yehu akakusanya watu wote na kuwaambia: “Ahabu alimwabudu Baali kwa kiwango kidogo tu.+ Lakini Yehu atamwabudu kwa kiwango kikubwa. 19 Basi sasa waiteni kwangu manabii+ wote wa Baali, waabudu+ wake wote na makuhani+ wake wote. Msiache hata mmoja akose kuwapo, kwa sababu nina dhabihu kubwa kwa ajili ya Baali. Yeyote atakayekosa kuwapo hataendelea kuishi.” Kwa habari ya Yehu, yeye alitenda kwa ujanja,+ kusudi awaharibu waabudu wa Baali.
20 Na Yehu akaendelea kusema: “Takaseni kusanyiko kuu kwa ajili ya Baali.” Basi wakalitangaza. 21 Kisha Yehu akatuma ujumbe katika Israeli yote,+ hivi kwamba waabudu wote wa Baali wakaja. Hakuna hata mmoja aliyebaki ambaye hakuja. Nao wakaendelea kuingia katika nyumba ya Baali,+ na nyumba ya Baali ikajaa kutoka mwisho mpaka mwisho. 22 Sasa akamwambia yule aliyesimamia chumba cha nguo: “Toa mavazi kwa ajili ya waabudu wote wa Baali.” Basi akawatolea mavazi. 23 Ndipo Yehu akaingia na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu katika nyumba ya Baali. Sasa akawaambia waabudu wa Baali: “Tafuteni kwa uangalifu mhakikishe kwamba hamna hapa ndani pamoja nanyi waabudu wowote wa Yehova, isipokuwa tu waabudu wa Baali.”+ 24 Mwishowe wakaingia ili kutoa dhabihu na matoleo ya kuteketezwa, na Yehu akaweka watu 80 upande wa nje ili wawepo kwa ajili yake, naye akaendelea kusema: “Mtu yeyote atakayeponyoka kati ya watu ninaotia mikononi mwenu, nafsi ya huyo mtu itakuwa badala ya nafsi ya yule mwingine.”+
25 Na ikawa kwamba mara tu alipomaliza kutoa lile toleo la kuteketezwa, Yehu akawaambia mara moja wale wakimbiaji na maamiri wasaidizi: “Ingieni ndani, wapigeni na kuwaua! Msiache hata mmoja atoke nje.”+ Na wale wakimbiaji na maamiri wasaidizi+ wakaanza kuwapiga na kuwaua kwa makali ya upanga na kuwatupa nje, nao wakazidi kwenda mpaka kwenye jiji la nyumba ya Baali. 26 Kisha wakazitoa nje nguzo takatifu+ za nyumba ya Baali na kuteketeza+ kila moja kwa moto. 27 Tena wakabomoa nguzo takatifu ya Baali+ na kuibomoa nyumba ya Baali,+ nao wakaitenga iwe choo+ mpaka leo hii.
28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza Baali kutoka katika Israeli. 29 Ni dhambi tu za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi,+ ambazo Yehu hakugeuka asizifuate, yaani, wale ndama wa dhahabu+ ambao mmoja alikuwa katika Betheli na mwingine katika Dani.+ 30 Basi Yehova akamwambia Yehu: “Kwa kuwa umetenda vema kwa kufanya yaliyo sawa machoni pangu,+ nawe umeitendea nyumba ya Ahabu+ kulingana na yote yaliyokuwa moyoni mwangu, wana, kufikia kizazi cha nne, wataketi kwa ajili yako juu ya kiti cha ufalme cha Israeli.”+ 31 Na Yehu hakuwa mwangalifu ili atembee katika sheria ya Yehova, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote.+ Yeye hakugeuka kutoka katika dhambi za Yeroboamu alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+
32 Siku hizo Yehova akaanza kukatilia mbali Israeli kipande kimoja baada ya kingine; na Hazaeli+ akaendelea kuwapiga katika eneo lote la Israeli, 33 kutoka Yordani kuelekea mashariki, nchi yote ya Gileadi,+ Wagadi+ na Warubeni+ na Wamanase,+ kutoka Aroeri,+ lililoko kando ya bonde la mto la Arnoni, naam, Gileadi na Bashani.+
34 Na mambo mengine ya Yehu na yote aliyofanya na uwezo wake wote, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 35 Mwishowe Yehu akalala pamoja na mababu+ zake, nao wakamzika katika Samaria; na Yehoahazi+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 36 Na siku ambazo Yehu alitawala juu ya Israeli zilikuwa miaka 28 katika Samaria.