2 Wafalme
9 Na Elisha nabii akamwita mmoja wa wana+ wa manabii, kisha akamwambia: “Jifunge viuno+ vyako uchukue chupa+ hii ya mafuta mkononi mwako, uende Ramothi-gileadi.+ 2 Utakapoingia humo, mwone Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi humo; nawe uingie ndani na kumsimamisha kutoka katikati ya ndugu zake, umwingize katika chumba cha ndani kabisa.+ 3 Nawe uchukue chupa ya mafuta uyamimine juu ya kichwa+ chake na kusema, ‘Yehova amesema hivi: “Ninakutia mafuta+ uwe mfalme+ juu ya Israeli.”’ Nawe ufungue mlango, ukimbie, wala usingoje.”
4 Na yule mtumishi, mtumishi wa nabii, akaondoka kwenda Ramothi-gileadi. 5 Alipoingia, tazama, wakuu wa majeshi walikuwa wameketi. Akasema: “Nina neno kwa ajili yako,+ ewe mkuu.” Ndipo Yehu akasema: “Ni kwa ajili ya nani kati yetu sote?” Kisha akasema: “Kwa ajili yako, ewe mkuu.” 6 Basi akasimama, akaingia ndani ya nyumba; naye akamimina yale mafuta juu ya kichwa chake na kumwambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme+ juu ya watu wa Yehova,+ yaani, juu ya Israeli. 7 Nawe uipige nyumba ya Ahabu bwana wako, nami lazima nilipize kisasi+ damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Yehova mkononi mwa Yezebeli.+ 8 Na nyumba yote ya Ahabu lazima iangamie; nami nitakatilia mbali kutoka kwa Ahabu+ mtu yeyote anayekojoa ukutani+ na yeyote asiye na uwezo na asiye na thamani+ katika Israeli. 9 Nami nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya. 10 Na mbwa watamla+ Yezebeli katika sehemu ya shamba kule Yezreeli, wala hakuna atakayemzika.’” Kisha akafungua mlango, akakimbia.+
11 Ndipo Yehu akatoka nje, akawaendea watumishi wa bwana wake, nao wakaanza kumuuliza: “Je, ni salama?+ Kwa nini huyu mwenda-wazimu+ alikuja kwako?” Lakini akawaambia: “Ninyi mnajua vema mtu huyo na namna yake ya kuongea.” 12 Lakini wakasema: “Si kweli! Tafadhali tuambie.” Ndipo akasema: “Aliniambia hivi na vile, akisema, ‘Yehova amesema hivi: “Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.”’”+ 13 Kwa hiyo wakafanya haraka, kila mmoja wao akachukua vazi+ lake na kulitandika chini yake juu ya zile ngazi zilizo wazi, nao wakaanza kupiga baragumu,+ wakisema: “Yehu amekuwa mfalme!”+ 14 Na Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi+ akapanga hila+ juu ya Yehoramu.
Na Yehoramu alikuwa akilinda kule Ramothi-gileadi,+ yeye na Israeli wote, kwa sababu ya Hazaeli+ mfalme wa Siria. 15 Baadaye Yehoramu+ mfalme akarudi kule Yezreeli+ ili apone yale majeraha ambayo Wasiria walimtia alipopigana na Hazaeli mfalme wa Siria.+
Sasa Yehu akasema: “Nafsi yenu ikikubali,+ msiache yeyote akimbie kutoka jijini na kupeleka habari Yezreeli.” 16 Na Yehu akaanza kupanda, akaenda Yezreeli; kwa maana Yehoramu alikuwa amelala huko, na Ahazia+ mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka kwenda kumwona Yehoramu. 17 Na mlinzi+ alikuwa amesimama juu ya mnara+ katika Yezreeli,+ naye akaona umati unaosukasuka wa watu wa Yehu alipokuwa akija, naye akasema mara moja: “Ninaona umati unaosukasuka wa watu.” Ndipo Yehoramu akasema: “Chukua askari mpanda-farasi, umtume awapokee, naye aseme, ‘Je, kuna amani?’”+ 18 Basi mpanda-farasi akaenda kumpokea na kusema: “Mfalme amesema hivi, ‘Je, kuna amani?’” Lakini Yehu akasema: “Una nini na ‘amani’?+ Nenda nyuma yangu!”
Na yule mlinzi+ akaendelea kutoa habari, akisema: “Yule mjumbe aliwafikia, lakini hakurudi.” 19 Kwa hiyo akatuma mpanda-farasi wa pili, ambaye, alipowafikia, alisema: “Mfalme amesema hivi, ‘Je, kuna amani?’” Lakini Yehu akasema: “Una nini na ‘amani’?+ Nenda nyuma yangu!”
20 Na yule mlinzi akaendelea kutoa habari, akisema: “Aliwafikia, lakini hakurudi; na uendeshaji ule ni kama uendeshaji wa Yehu+ mjukuu wa Nimshi,+ kwa maana yeye huendesha kiwazimu.”+ 21 Ndipo Yehoramu akasema: “Fungeni!”+ Basi gari lake la vita likafungwa, na Yehoramu mfalme wa Israeli na Ahazia+ mfalme wa Yuda wakatoka, kila mmoja wao akiwa ndani ya gari lake la vita. Walipoendelea kwenda kumpokea Yehu, wakamkuta katika sehemu ya shamba la Nabothi,+ Myezreeli.
22 Na ikawa kwamba mara tu Yehoramu alipomwona Yehu, mara moja akasema: “Je, kuna amani, Yehu?” Lakini yeye akasema: “Kunaweza kuwa na amani+ gani wakati kungali na uasherati wa Yezebeli+ mama yako na ulozi wake mwingi?”+ 23 Mara moja Yehoramu akageuka kwa mikono yake, ili akimbie, na kumwambia Ahazia: “Kuna udanganyifu,+ Ahazia!” 24 Na Yehu akatia upinde+ mkononi mwake, akampiga Yehoramu katikati ya mikono, hivi kwamba ule mshale ukatokea moyoni mwake, naye akaanguka ndani ya gari lake la vita.+ 25 Sasa akamwambia Bidkari amiri msaidizi wake:+ “Mwinue; mtupe katika ile sehemu ya shamba la Nabothi, Myezreeli;+ kwa maana kumbuka: Mimi na wewe tulikuwa tukiendesha makundi ya magari ya farasi nyuma ya Ahabu baba yake, na Yehova akatangaza+ hivi juu yake: 26 ‘ “Hakika niliona jana damu+ ya Nabothi na damu ya wanawe,”+ asema Yehova, “nami hakika nitakulipa+ wewe katika sehemu hii ya shamba,” asema Yehova.’ Basi sasa, mwinue; mtupe katika ile sehemu ya shamba kulingana na neno la Yehova.”+
27 Na Ahazia+ mfalme wa Yuda akaona hilo, akaanza kukimbia kupitia njia ya bustani ya nyumba.+ (Baadaye Yehu akamfuatilia na kusema: “Yeye pia! Mpigeni!” Kwa hiyo wakampiga alipokuwa ndani ya gari kwenye njia inayopanda kwenda Guri, lililo kando ya Ibleamu.+ Naye akaendelea kukimbia kwenda Megido,+ akafa huko.+ 28 Ndipo watumishi wake wakambeba ndani ya gari mpaka Yerusalemu, na hivyo wakamzika katika kaburi lake pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 29 Na ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja wa Yehoramu+ mwana wa Ahabu kwamba Ahazia+ alianza kuwa mfalme juu ya Yuda.)
30 Mwishowe Yehu akafika Yezreeli,+ na Yezebeli+ akasikia habari hizo. Naye akapaka macho yake wanja+ na kukipamba kichwa chake,+ akatazama chini kupitia dirishani.+ 31 Na Yehu akaingia kupitia lango. Basi yule mwanamke akasema: “Je, mambo yalimwendea sawa Zimri,+ aliyemuua bwana wake?” 32 Basi akainua uso wake kuelekea lile dirisha na kusema: “Ni nani aliye pamoja nami? Ni nani?”+ Mara moja maofisa+ wawili au watatu wa makao ya mfalme wakaangalia chini kumtazama. 33 Basi akasema: “Mwangusheni!”+ Ndipo wakamwangusha huyo mwanamke, na sehemu ya damu yake ikamwagika juu ya ukuta na juu ya farasi; naye akamkanyaga-kanyaga.+ 34 Kisha akaingia ndani, akala na kunywa na kisha kusema: “Tafadhali, mshughulikieni mtu huyu aliyelaaniwa+ na mkamzike, kwa maana yeye ni binti ya mfalme.”+ 35 Walipoenda kumzika, hawakupata chochote chake isipokuwa fuvu la kichwa na miguu na viganja vya mikono.+ 36 Waliporudi na kumwambia, ndipo akasema: “Hilo ni neno la Yehova alilosema kupitia+ mtumishi wake Eliya, Mtishbi, kusema, ‘Katika sehemu ya shamba la Yezreeli mbwa wataila nyama ya Yezebeli.+ 37 Na maiti ya Yezebeli itakuwa kama mbolea+ juu ya uso wa shamba katika sehemu ya shamba la Yezreeli, ili wasiseme: “Huyu ni Yezebeli.”’”+