29 Kwa hiyo Yehoramu+ mfalme akarudi Yezreeli+ ili apone yale majeraha waliyomtia Wasiria kule Rama alipopigana na Hazaeli mfalme wa Siria. Naye Ahazia+ mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka ili amwone Yehoramu mwana wa Ahabu katika Yezreeli, kwa maana alikuwa mgonjwa.
7 Lakini kuanguka+ kwa Ahazia kulitokana na Mungu,+ alipomjia Yehoramu; naye alipokuja, alienda+ pamoja na Yehoramu kwa Yehu+ mjukuu wa Nimshi,+ ambaye Yehova alikuwa amemtia mafuta+ ili aikatilie mbali nyumba ya Ahabu.+