21Na ikawa kwamba baada ya mambo hayo palikuwa na shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, lililokuwa kule Yezreeli,+ kando ya jumba la mfalme Ahabu, mfalme wa Samaria.
15 Na ikawa kwamba mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa kwa mawe akafa, mara moja Yezebeli akamwambia Ahabu: “Ondoka, miliki shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli,+ ambalo alikataa kukupa kwa pesa; kwa maana Nabothi hayuko hai tena, bali amekufa.”
19 Nawe unapaswa kumwambia, ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Je, umeua+ na pia ukamiliki?”’+ Nawe unapaswa kumwambia, ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Mahali+ ambapo mbwa waliiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, ndiyo, damu yako.”’”+