12 “Wakati wowote unapowahesabu wana wa Israeli,+ basi kila mmoja wao atamtolea Yehova fidia kwa ajili ya nafsi yake wakati wa kuhesabiwa kwao,+ ili kusiwe na pigo juu yao wakati wa kuhesabiwa kwao.+
13 Hiki ndicho watakachotoa wale wote wanaopita kwa wale waliohesabiwa: nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.+ Gera 20 zinatoshana na shekeli moja. Nusu shekeli ndio mchango kwa Yehova.+
16 Nawe utachukua pesa za fedha za upatanisho kutoka kwa wana wa Israeli na kuzitoa kwa ajili ya utumishi wa hema la mkutano,+ ili kwa kweli uwe ukumbusho mbele za Yehova na wana wa Israeli, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”