5 “‘Kisha yule ng’ombe-dume mchanga atachinjwa mbele za Yehova; na wana wa Haruni, makuhani,+ wataitoa damu na kuinyunyiza damu hiyo kwenye madhabahu kuizunguka pande zote,+ madhabahu iliyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
18 Naye atatia sehemu ya damu hiyo juu ya pembe za madhabahu+ iliyo mbele za Yehova, ambayo imo ndani ya hema la mkutano; na damu yote inayobaki ataimimina kwenye msingi wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa,+ iliyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano.