9 na bado nilipokuwa pamoja nanyi na nikapatwa na uhitaji, sikuwa mzigo kwa mtu hata mmoja,+ kwa maana ndugu waliotoka Makedonia+ walijazia kwa wingi upungufu wangu. Ndiyo, katika kila njia nilikaa mwenyewe bila kuwa mzigo kwenu nami nitakaa hivyo.+
14 Tazama! Hii ndiyo mara ya tatu+ niliyo tayari kuja kwenu, na bado sitakuwa mzigo. Kwa maana ninatafuta, si mali zenu,+ bali ninyi; kwa maana watoto+ hawapaswi kuweka akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi kwa ajili ya watoto wao.+