9 Mfalme akiona vema, na iandikwe kwamba waharibiwe; nami nitalipa talanta elfu kumi+ za fedha mikononi mwa wale wanaofanya kazi+ hiyo kwa kuzileta katika hazina ya mfalme.”
7 Ndipo Mordekai akamweleza kuhusu mambo yote yaliyompata+ na taarifa kamili ya pesa ambazo Hamani alikuwa amesema atalipa kwa hazina+ ya mfalme juu ya Wayahudi, ili kuwaangamiza.+
8 Naye akampa nakala+ ya maandishi ya sheria ya kuwaangamiza iliyokuwa imetolewa Shushani+ ili amwonyeshe Esta na kumweleza na kumwagiza+ kwamba aingie kwa mfalme na kumwomba kibali+ na kutoa ombi moja kwa moja mbele yake kwa ajili ya watu wake mwenyewe.+