Esta
4 Basi Mordekai+ akapata kujua mambo yote yaliyokuwa yamefanywa;+ ndipo Mordekai akararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia+ na majivu,+ akaenda katikati ya jiji, akalia kwa sauti kubwa na yenye uchungu.+ 2 Mwishowe akaja mpaka mbele ya lango la mfalme,+ kwa maana hakuna yeyote aliyepaswa kuingia katika lango la mfalme akiwa amevaa nguo za magunia. 3 Na katika wilaya zote mbalimbali za utawala,+ kokote ambako neno la mfalme na sheria yake ilikuwa ikifika, kulitokea maombolezo+ makubwa kati ya Wayahudi, na kufunga,+ na kulia, na kuomboleza. Na wengi wakatandika nguo za magunia+ na majivu+ kuwa vitanda vyao. 4 Na wanawake vijana wa Esta na matowashi+ wake wakaingia na kumpa habari. Na malkia akaumia sana. Kisha akaagiza mavazi ya kumvika Mordekai yapelekwe na nguo zake za magunia zivuliwe. Naye hakuyakubali.+ 5 Kisha Esta akamwita Hathaki,+ mmoja wa matowashi wa mfalme, ambaye mfalme alikuwa amemweka amhudumie Esta, akampa amri kumhusu Mordekai, apate kuyajua mambo hayo na maana yake.
6 Basi Hathaki akaenda kwa Mordekai kwenye kiwanja cha watu wote cha jiji kilichokuwa mbele ya lango la mfalme. 7 Ndipo Mordekai akamweleza kuhusu mambo yote yaliyompata+ na taarifa kamili ya pesa ambazo Hamani alikuwa amesema atalipa kwa hazina+ ya mfalme juu ya Wayahudi, ili kuwaangamiza.+ 8 Naye akampa nakala+ ya maandishi ya sheria ya kuwaangamiza iliyokuwa imetolewa Shushani+ ili amwonyeshe Esta na kumweleza na kumwagiza+ kwamba aingie kwa mfalme na kumwomba kibali+ na kutoa ombi moja kwa moja mbele yake kwa ajili ya watu wake mwenyewe.+
9 Basi Hathaki+ akaingia na kumwambia Esta maneno ya Mordekai. 10 Ndipo Esta akamwambia Hathaki na kumwamuru hivi kumhusu Mordekai:+ 11 “Watumishi wote wa mfalme na watu wa wilaya za utawala wa mfalme wanajua kwamba mwanamume au mwanamke yeyote anayeingia kwa mfalme katika ua wa ndani+ bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu,+ kwamba mtu huyo auawe; ila tu mfalme akimnyooshea fimbo yake ya enzi ya dhahabu, ndipo atakapoendelea kuishi.+ Lakini mimi, kwa siku 30 sasa sijaitwa kuingia kwa mfalme.”
12 Nao wakamwambia Mordekai maneno ya Esta. 13 Ndipo Mordekai akasema Esta apewe jibu hili: “Usiwaze katika nafsi yako mwenyewe kwamba nyumba ya mfalme itaponyoka kuliko Wayahudi wengine wote.+ 14 Kwa maana ukinyamaza kabisa wakati huu, msaada na ukombozi wa Wayahudi utasimama kutoka mahali pengine;+ bali wewe pamoja na nyumba ya baba yako, mtaangamizwa. Na ni nani anayejua ikiwa si kwa ajili ya wakati kama huu kwamba umefikia heshima ya kifalme?”+
15 Basi Esta akasema Mordekai apewe jibu la kusema: 16 “Nenda, wakusanye Wayahudi wote waliopo Shushani+ na mfunge+ kwa ajili yangu, msile wala kunywa kwa siku tatu,+ usiku na mchana. Mimi pia pamoja na wanawake wangu vijana,+ nitafunga vivyo hivyo, na baada ya hapo nitaingia kwa mfalme, jambo ambalo ni kinyume cha sheria. Nami nikiangamia,+ na niangamie.” 17 Kwa hiyo Mordekai akaenda zake na kufanya kulingana na yote ambayo Esta alikuwa amemwamuru.