10 Na itakuwa katika siku hiyo+ kwamba patakuwa na mzizi wa Yese+ ambao utakuwa unasimama kuwa ishara kwa ajili ya vikundi vya watu.+ Mataifa yatamtafuta yeye ili kuuliza habari zake,+ na mahali pake pa kupumzikia patakuwa patukufu.+
2 Na kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na dhoruba ya mvua,+ kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,+ kama kivuli cha mwamba mzito katika nchi iliyochoka.+