30 Utamchumbia mwanamke, lakini mwanamume mwingine atamlala kinguvu.+ Utajenga nyumba, lakini hutakaa ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutaanza kutumia matunda yake.+
13 Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+ Wamefanya kazi mpaka wakawa wagonjwa; hawatakuwa na faida yoyote.+ Nao hakika wataona aibu kwa ajili ya mazao yenu kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.”
13 Na mali yao itakuwa ya kunyakuliwa na nyumba zao zitakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nao watajenga nyumba, lakini hawatakaa humo;+ nao watapanda mashamba ya mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+