Hosea
8 “Tia baragumu+ katika kinywa chako! Mtu fulani anakuja kama tai+ juu ya nyumba ya Yehova, kwa sababu wamelivunja agano langu,+ nao wameikosea sheria yangu.+ 2 Wao wanazidi kunililia, ‘Ee Mungu wangu, sisi, Israeli, tumekujua.’+
3 “Israeli ametupilia mbali wema.+ Adui na amfuatilie.+ 4 Wao wenyewe wameweka wafalme,+ lakini si kwa sababu yangu. Wameweka wakuu, lakini mimi sikuwa na habari. Wamejifanyia sanamu+ kwa fedha yao na dhahabu yao, kusudi wakatiliwe mbali.+ 5 Ndama wako ametupiliwa mbali,+ Ee Samaria. Hasira yangu imewaka juu yao.+ Wataendelea mpaka wakati gani kutoweza kuwa na hali isiyo na hatia?+ 6 Kwa maana katika Israeli kimetokea hata kitu hiki.+ Fundi tu ndiye aliyekifanya,+ wala si Mungu; kwa maana ndama wa Samaria atavunjika vipande-vipande.+
7 “Kwa maana wao huendelea kupanda upepo, nao watavuna+ upepo wa dhoruba. Hakuna chochote chenye nafaka inayosimama.+ Hakuna chipukizi lolote linalotoa unga.+ Chipukizi lolote likiutokeza, wageni wataumeza.+
8 “Israeli watamezwa.+ Sasa watakuja kuwa kati ya mataifa,+ kama chombo ambacho hakipendezi.+ 9 Kwa maana wao wenyewe wamepanda kwenda Ashuru,+ kama punda-milia aliyejitenga.+ Kwa habari ya Efraimu, wamekodi wapenzi.+ 10 Pia, ingawa wanaendelea kuwakodi kati ya mataifa,+ sasa mimi nitawakusanya pamoja; nao watakuwa katika maumivu makali+ kwa kitambo kidogo kwa sababu ya mzigo wa mfalme na wakuu.
11 “Kwa maana Efraimu amezidisha madhabahu ili kutenda dhambi.+ Amekuwa na madhabahu ili atende dhambi.+ 12 Ndipo nikamwandikia mambo mengi ya sheria yangu;+ nayo yamehesabiwa kuwa kama kitu kigeni.+ 13 Walizidi kunitolea dhabihu ya nyama kuwa dhabihu za zawadi,+ nao wakaendelea kula vitu ambavyo Yehova hakufurahia.+ Sasa atakumbuka kosa lao na kutoza hesabu kwa sababu ya dhambi zao.+ Ndipo wao waliporudi Misri.+ 14 Naye Israeli akaanza kumsahau Mtengenezaji wake+ na kujenga mahekalu;+ naye Yuda akazidisha majiji yenye ngome.+ Nami nitapeleka moto katika majiji yake nao utateketeza minara ya makao ya kila mmoja.”+