19 Ee matumbo yangu, matumbo yangu! Nina maumivu makali katika kuta za moyo wangu.+ Moyo wangu umechafuka ndani yangu.+ Siwezi kunyamaza kimya, kwa maana nafsi yangu imesikia sauti ya baragumu, king’ora cha vita.+
22 Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zao, utakapoleta juu yao kwa ghafula kikundi cha waporaji.+ Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata, nao wameficha mitego kwa ajili ya miguu yangu.+