15 Nawe utasema naye na kuyaweka maneno hayo kinywani mwake;+ nami nitakuwa pamoja na kinywa chako na kinywa chake,+ nami nitawafundisha mambo mtakayofanya.+
16 Nami nitayatia maneno yangu katika kinywa chako,+ na hakika mimi nitakufunika kwa kivuli cha mkono wangu,+ ili kuzipanda mbingu+ na kuuweka msingi wa dunia+ na kuuambia Sayuni, ‘Ninyi ni watu wangu.’+
7 “Basi kwa habari yako wewe, Ee mwana wa binadamu, nimekufanya kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli,+ na kutoka katika kinywa changu lazima usikie neno na kuwapa onyo kutoka kwangu.+