4 Na Yeremia akamwita Baruku+ mwana wa Neria ili Baruku aandike kwa kinywa cha Yeremia maneno yote ya Yehova ambayo Yeye alikuwa amemwambia, katika kile kitabu cha kukunjwa.+
26 Na zaidi ya hayo, mfalme akawaamuru Yerahmeeli mwana wa mfalme na Seraya mwana wa Azrieli na Shelemia mwana wa Abdeeli waende kumleta Baruku mwandishi na Yeremia nabii.+ Lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+