9 Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyekuwa amewatoa mababu zao katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia. Ndiyo sababu Yehova alileta juu yao msiba huu wote.’”+
18 Je, mababu zenu hawakufanya hivyo,+ hivi kwamba Mungu akaleta juu yetu msiba huu wote,+ na pia juu ya jiji hili? Na bado mnaiongeza hasira inayowaka juu ya Israeli kwa kuitia sabato unajisi.”+
11 Na watu wote wa Israeli wamevunja sheria yako, wamegeuka kando kwa kutotii sauti yako,+ hata ukatumwagia laana na kiapo rasmi+ ambacho kimeandikwa katika sheria ya Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, kwa maana tumemtendea Yeye dhambi.