8 Na katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi huo, yaani, mwaka wa kumi na tisa+ wa Mfalme Nebukadneza mfalme wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babiloni, aliingia ndani ya Yerusalemu.+
9 Na Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi+ akawapeleka uhamishoni kule Babiloni+ wale watu wengine walioachwa ndani ya jiji, na wale waliokimbia ili kujiunga naye, na watu wengine walioachwa.
40Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova baada ya Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi kumtoa katika Rama,+ alipomchukua huku akiwa amefungwa kwa pingu za mkononi katikati ya wahamishwa wote wa Yerusalemu na wa Yuda, ambao walikuwa wakipelekwa uhamishoni katika Babiloni.+