16 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jichukulie kijiti+ na uandike juu yake, ‘Kwa Yuda na kwa wenzake, wana wa Israeli.’+ Na uchukue kijiti kingine na kuandika juu yake, ‘Kwa Yosefu, kijiti cha Efraimu,+ na wenzake, nyumba yote ya Israeli.’+
6 Nami nitaifanya nyumba ya Yuda iwe kuu, nami nitaiokoa nyumba ya Yosefu.+ Nami nitawapa makao, kwa maana nitawaonyesha rehema;+ nao watakuwa kama watu ambao sikutupilia mbali;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, nami nitawajibu.+