Zekaria
10 “Mwombeni Yehova mvua+ wakati wa mvua ya masika,+ Yehova anayefanya mawingu ya dhoruba,+ ambaye huwapa mvua kubwa,+ na kumpa kila mmoja mimea shambani.+ 2 Kwa maana terafimu+ zimesema mambo ya uchawi; nao waaguzi wameona maono ya uwongo,+ nao huendelea kusema ndoto za bure, nao hujaribu kufariji kwa ubatili.+ Ndiyo sababu wataondoka kama kundi;+ watateseka, kwa sababu hakuna mchungaji.+
3 “Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji,+ nami nitawatoza hesabu+ viongozi walio kama mbuzi;+ kwa maana Yehova wa majeshi ameelekeza fikira zake kwa kundi lake,+ nyumba ya Yuda, naye amewafanya kama farasi+ wake mwenye heshima katika mapigano. 4 Kutoka kwake kuna mkuu,+ kutoka kwake kuna mtawala anayetegemeza,+ kutoka kwake kuna upinde wa mapigano;+ kwake hutoka kila msimamizi wa kazi,+ wote pamoja. 5 Nao watakuwa kama wanaume wenye nguvu+ wanaokanyaga matope ya barabarani katika mapigano.+ Nao watajihusisha katika mapigano, kwa maana Yehova yupo pamoja nao;+ na hao wapanda-farasi wataona aibu.+ 6 Nami nitaifanya nyumba ya Yuda iwe kuu, nami nitaiokoa nyumba ya Yosefu.+ Nami nitawapa makao, kwa maana nitawaonyesha rehema;+ nao watakuwa kama watu ambao sikutupilia mbali;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, nami nitawajibu.+ 7 Na wale wa Efraimu watakuwa kama mwanamume mwenye nguvu,+ na moyo wao utashangilia kana kwamba kutokana na divai.+ Na wana wao wenyewe wataona nao hakika washangilie;+ moyo wao utashangilia katika Yehova.+
8 “ ‘Nitawapigia mluzi+ na kuwakusanya pamoja; kwa maana nitawakomboa,+ nao watakuwa wengi, kama wale ambao wamekuwa wengi.+ 9 Nami nitawatawanya kama mbegu katikati ya mataifa,+ nao watanikumbuka wakiwa mbali;+ nao wataamka pamoja na wana wao na kurudi.+ 10 Nami nitawarudisha kutoka nchi ya Misri;+ nitawakusanya pamoja kutoka Ashuru;+ nami nitawaleta katika nchi ya Gileadi+ na Lebanoni, wala nafasi haitapatikana kwa ajili yao.+ 11 Naye atapita baharini kwa taabu;+ na ndani ya bahari atayapiga mawimbi,+ na vilindi vyote vya Nile vitakauka.+ Nacho kiburi cha Ashuru kitashushwa,+ na fimbo ya enzi+ ya Misri itaondoka.+ 12 Nami nitawafanya wawe wakuu katika Yehova,+ nao watatembea huku na huku katika jina lake,’+ asema Yehova.”