17 Badala ya shaba nitaingiza dhahabu,+ na badala ya chuma nitaingiza fedha, na badala ya miti, shaba, na badala ya mawe, chuma; nami nitaweka amani kuwa waangalizi+ wako na uadilifu kuwa wagawa-kazi wako.+
17 ‘Hakika macho yako na moyo wako haviko juu ya chochote ila pato lisilo la haki,+ na juu ya damu ya asiye na hatia ili kuimwaga,+ na juu ya kupunja na juu ya unyang’anyi ili kuyaendeleza mambo hayo.’
5 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamsimamishia Daudi chipukizi adilifu.+ Na hakika mfalme atatawala+ na kutenda kwa busara na kutenda haki na uadilifu katika nchi.+
27 Wakuu wake walio katikati yake ni kama mbwa-mwitu wanaorarua mawindo katika kumwaga damu,+ katika kuangamiza nafsi kusudi wapate pato lisilo la haki.+
18 Naye mkuu hatachukua urithi wowote wa watu ili kuwalazimisha waondoke katika miliki yao.+ Atawapa wanawe urithi kutoka kwenye miliki yake mwenyewe, ili watu wangu wasitawanyike kila mmoja mbali na miliki yake.’ ”+