3 Kwa maana, “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitawakusanya mateka wa watu wangu, Israeli na Yuda,”+ Yehova amesema, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao hakika wataimiliki tena.”’”+
14 “Kwa hiyo toa unabii, Ee mwana wa binadamu, nawe umwambie Gogu, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Je, haitakuwa katika siku ile wakati watu wangu Israeli wanapokaa kwa usalama kwamba utajua hilo?+
20 Wakati huo nitawaleta ndani ninyi, hata wakati wangu wa kuwakusanya ninyi pamoja. Kwa maana nitawafanya ninyi kuwa jina na sifa kati ya vikundi vyote vya watu wa dunia, ninapowakusanya ili kuwarudisha mateka wenu mbele ya macho yenu,” Yehova amesema.+