3 ndipo Yehova Mungu wako atakaporudisha mateka+ wako pia na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka kwa vikundi vyote vya watu ambako Yehova Mungu wako amekutawanya.+
22 ‘ “Vitapelekwa Babiloni+ navyo vitaendelea kuwa huko mpaka siku ile nitakapovikazia fikira,”+ asema Yehova. “Nami nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+
14 Nami nitajiacha mnipate,’+ asema Yehova. ‘Nami nitakusanya kundi lenu la mateka na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na kutoka katika mahali pote ambapo nimewatawanya ninyi,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawarudisha katika mahali ambapo kutoka hapo niliwapeleka uhamishoni.’+
25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Sasa nitawarudisha mateka wa Yakobo+ na kwa kweli niwe na rehema juu ya nyumba yote ya Israeli;+ nami nitajitoa kikamili kwa ajili ya jina langu takatifu.+
14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+