Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 62:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Yehova ameapa kwa mkono wake wa kuume+ na kwa mkono wake wenye nguvu:+ “Sitawapa tena adui zako nafaka yako iwe chakula,+ wala wageni hawatakunywa divai yako mpya,+ ambayo umeifanyia kazi.

  • Yeremia 30:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,” asema Yehova, “wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa wewe kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yao ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi na kuwa huru kutokana na usumbufu naye atastarehe, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayemtetemesha.”+

  • Ezekieli 28:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nao kwa kweli watakaa juu yake kwa usalama+ na kujenga nyumba+ na kupanda mashamba ya mizabibu,+ nao watakaa kwa usalama+ ninapofanya matendo ya hukumu juu ya wale wote wanaowatendea kwa dhihaka kuwazunguka pande zote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao.” ’ ”

  • Mika 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Nao wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake,+ wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha;+ kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki