3 Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi na apande na kwenda Yerusalemu, huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli+—iliyokuwa Yerusalemu.+
8 Neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ambaye anawakusanya waliotawanyika wa Israeli,+ ni hili: “Nitawakusanya pamoja kwake wengine mbali na wale walio wake ambao tayari wamekusanywa.”+
37 ‘Tazama, ninawakusanya pamoja kutoka katika nchi zote ambako nitakuwa nimewatawanya katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu na katika hasira kuu;+ nami nitawarudisha mahali hapa na kuwakalisha katika usalama.+
13 Nami nitawatoa+ kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika zile nchi na kuwaleta kwenye nchi yao+ na kuwalisha kwenye milima ya Israeli, kando ya vijito na kando ya makao yote ya nchi.+