147 Msifuni Yah,+
Kwa maana ni vema kumpigia Mungu wetu muziki;+
Kwa maana inapendeza—sifa inafaa.+
2 Yehova anajenga Yerusalemu;+
Huwakusanya pamoja waliotawanywa wa Israeli.+
3 Anawaponya+ wenye mioyo iliyovunjika,+
Naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.+
4 Anahesabu idadi ya nyota;+
Zote anaziita kwa majina yake.+
5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye nguvu nyingi;+
Uelewaji wake hauwezi kusimuliwa.+
6 Yehova anawatuliza wapole;+
Anawashusha waovu mpaka chini.+
7 Mwitikieni Yehova kwa kutoa shukrani;+
Mpigieni Yehova muziki kwenye kinubi,+
8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,+
Yeye anayetayarisha mvua kwa ajili ya dunia,+
Yeye anayefanya milima ichipushe majani mabichi.+
9 Anawapa wanyama chakula chao,+
Kunguru wachanga wanaoendelea kuita.+
10 Hapendezwi na nguvu za farasi,+
Wala hafurahii miguu ya mtu.+
11 Yehova anawafurahia wale wanaomwogopa,+
Wale wanaozingojea fadhili zake zenye upendo.+
12 Mpongeze Yehova,+ Ee Yerusalemu.
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.+
13 Kwa maana ameyatia nguvu mapingo ya lango lako;
Amewabariki wana wako katikati yako.+
14 Anaweka amani katika eneo lako;+
Anaendelea kukushibisha kwa unono wa ngano.+
15 Anayatuma maneno yake duniani;+
Neno lake hukimbia haraka.
16 Anatoa theluji kama sufu;+
Anatawanya sakitu kama majivu.+
17 Anatupa barafu yake kama matonge.+
Mbele ya baridi yake ni nani anayeweza kusimama?+
18 Anatuma neno lake+ na kuviyeyusha.
Huufanya upepo uvume;+
Maji hutiririka.
19 Anamtangazia Yakobo neno lake,+
Na Israeli masharti+ yake na maamuzi yake ya hukumu.+
20 Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote;+
Nao hawajajua maamuzi yake ya hukumu.+
Msifuni Yah!+