Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 106:47
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 47 Utuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+

      Na utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa+

      Ili tulishukuru jina lako takatifu,+

      Ili tukusifu kwa shangwe.+

  • Isaya 65:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Nami nitaleta uzao kutoka katika Yakobo+ na mrithi wa milima yangu kutoka katika Yuda;+ na wachaguliwa wangu wataumiliki,+ na watumishi wangu wenyewe watakaa huko.+

  • Yeremia 23:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Nami nitakusanya mabaki ya kondoo zangu kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye uwanja wao wa malisho,+ na hakika wao watazaa na kuwa wengi.+

  • Yeremia 30:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana, “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitawakusanya mateka wa watu wangu, Israeli na Yuda,”+ Yehova amesema, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao hakika wataimiliki tena.”’”+

  • Ezekieli 11:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 “Kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya ninyi kutoka katika nchi ambazo katikati yake mmetawanywa, nami nitawapa ninyi udongo wa Israeli.+

  • Ezekieli 28:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Nitakapokusanya pamoja nyumba ya Israeli kutoka kwa vikundi vya watu ambao kati yao wametawanyika,+ mimi pia nitatakaswa kati yao machoni pa mataifa.+ Nao hakika watakaa kwenye nchi+ yao niliyompa mtumishi wangu, Yakobo.+

  • Amosi 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki