Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 11:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na itatukia katika siku hiyo kwamba Yehova atatoa tena mkono wake, mara ya pili,+ ili kuchukua mabaki ya watu wake watakaobaki kutoka Ashuru+ na kutoka Misri+ na kutoka Pathrosi+ na kutoka Kushi+ na kutoka Elamu+ na kutoka Shinari+ na kutoka Hamathi na kutoka visiwa vya bahari.+

  • Yeremia 30:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,” asema Yehova, “wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa wewe kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yao ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi na kuwa huru kutokana na usumbufu naye atastarehe, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayemtetemesha.”+

  • Yeremia 32:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 ‘Tazama, ninawakusanya pamoja kutoka katika nchi zote ambako nitakuwa nimewatawanya katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu na katika hasira kuu;+ nami nitawarudisha mahali hapa na kuwakalisha katika usalama.+

  • Ezekieli 20:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 “ ‘Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ nitakapowaleta kwenye udongo wa Israeli,+ katika nchi ambayo niliuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa mababu zenu.

  • Ezekieli 34:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nami nitawatoa+ kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika zile nchi na kuwaleta kwenye nchi yao+ na kuwalisha kwenye milima ya Israeli, kando ya vijito na kando ya makao yote ya nchi.+

  • Ezekieli 36:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Nami nitawatoa ninyi kutoka kwa mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi zote na kuwaingiza katika nchi yenu.+

  • Ezekieli 37:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa hiyo toa unabii, nawe utawaambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama ninayafungua makaburi yenu,+ nami nitawatoa kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, na kuwaingiza katika nchi ya Israeli.+

  • Amosi 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki