4 Nao watajenga upya mahali palipoharibiwa kwa muda mrefu;+ watasimamisha mahali palipofanywa ukiwa pa nyakati za kale,+ nao hakika watajenga upya yale majiji yaliyoharibiwa,+ mahali palipofanywa ukiwa kwa kizazi baada ya kizazi.
33 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Siku nitakayowasafisha ninyi kutokana na makosa yenu yote nitayafanya pia majiji yakaliwe,+ na mahali palipoharibiwa patajengwa upya.+