Isaya
61 Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu,+ kwa sababu Yehova amenitia mafuta+ niwatangazie wapole habari njema.+ Amenituma kufunga majeraha ya waliovunjika moyo,+ kutangaza uhuru kwa wale waliochukuliwa mateka+ na kufunguliwa kabisa kwa macho hata kwa walio wafungwa;+ 2 kutangaza mwaka wa nia njema upande wa Yehova+ na siku ya kisasi upande wa Mungu wetu;+ kuwafariji wote wanaoomboleza;+ 3 kuwapa wale wanaoomboleza kwa ajili ya Sayuni, kuwapa vazi la kichwani badala ya majivu,+ mafuta ya furaha+ badala ya maombolezo, nguo ya kujitanda ya sifa badala ya roho iliyovunjika;+ nao wataitwa miti mikubwa ya uadilifu,+ bustani ya Yehova,+ ili yeye arembeshwe.+ 4 Nao watajenga upya mahali palipoharibiwa kwa muda mrefu;+ watasimamisha mahali palipofanywa ukiwa pa nyakati za kale,+ nao hakika watajenga upya yale majiji yaliyoharibiwa,+ mahali palipofanywa ukiwa kwa kizazi baada ya kizazi.
5 “Na wageni kwa kweli watasimama na kuchunga makundi yenu,+ na watu wa nchi nyingine+ watakuwa wakulima wenu na watunza-mizabibu wenu.+ 6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Yehova;+ itasemekana ninyi ni wahudumu wa Mungu wetu.+ Ninyi mtakula mali za mataifa,+ nanyi mtasema kujihusu ninyi wenyewe kwa kuchangamka katika utukufu wao.+ 7 Badala ya aibu yenu kutakuwa na fungu mara mbili,+ na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe juu ya fungu lao.+ Kwa hiyo watamiliki fungu mara mbili+ katika nchi yao. Watakuwa na shangwe mpaka wakati usio na kipimo.+ 8 Kwa maana mimi, Yehova, napenda haki,+ nachukia unyang’anyi pamoja na ukosefu wa uadilifu.+ Nami nitatoa malipo yao katika ukweli,+ nitafanya kwao agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.+ 9 Na uzao wao kwa kweli utajulikana katika mataifa, na wazao wao katikati ya vikundi vya watu.+ Wale wote wanaowaona watawatambua,+ kwamba wao ni uzao ambao Yehova amebariki.”+
10 Hakika nitafurahi katika Yehova.+ Nafsi yangu itakuwa na shangwe katika Mungu wangu.+ Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu;+ amenivika koti lisilo na mikono la uadilifu,+ kama bwana-arusi ambaye, kama kuhani, anavaa vazi la kichwani,+ na kama bibi-arusi anayejipamba kwa vitu vya mapambo yake.+ 11 Kwa maana kama vile dunia inavyotoa chipukizi lake, na kama vile bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa ndani yake,+ ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atakavyotoa chipukizi la uadilifu+ na la sifa mbele ya mataifa yote.+